Zaburi 101 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Ahadi ya mfalme juu ya uaminifu na hakiYa Daudi. Zaburi.

1Rehema na hukumu nitaziimba,

Ee BWANA, nitakuimbia zaburi.

2 1 Sam 18:14; Mwa 18:19; Kum 6:7; 1 Fal 9:4 Nitaiangalia njia ya unyofu;

Utakuja kwangu lini?

Nitakwenda kwa unyofu wa moyo

Ndani ya nyumba yangu.

3 Yos 23:6; 1 Sam 12:20 Sitaweka mbele ya macho yangu

Neno la uovu.

Kazi yao waliopotoka naichukia,

Haitaambatana nami.

4 Mt 7:23; 1 Kor 5:11; 2 Tim 2:19 Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu,

Lililo ovu sitalijua.

5 Mit 6:17; Lk 18:14 Amsingiziaye jirani yake kwa siri,

Huyo nitamwangamiza.

Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno,

Huyo sitamvumilia.

6 Rum 13:4 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,

Hao wakae nami.

Yeye aendaye katika njia kamilifu,

Ndiye atakayenitumikia.

7Hatakaa ndani ya nyumba yangu

Mtu atendaye hila.

Asemaye uongo hatathibitika

Mbele ya macho yangu.

8 Yer 21:12; Hos 9:3 Kila asubuhi nitawaangamiza

Waovu wote nchini.

Nikiwatenga wote watendao uovu

Na mji wa BWANA.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help