Zaburi 15 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Nani atakaa katika patakatifu pa Mungu?Zaburi ya Daudi.

1 Zab 2:5 BWANA, ni nani atakayekaa

Katika hema yako?

Ni nani atakayeishi

Katika kilima chako kitakatifu?

2 Zab 84:11; Isa 33:15,16 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,

Na kutenda haki.

Asemaye kweli kwa moyo wake,

3Asiyesingizia kwa ulimi wake.

Wala kumtenda mwenziwe mabaya,

Wala kumsengenya jirani yake.

4 Yos 9:18-20 Anayedharau waovu Machoni pake,

Bali huwaheshimu wamchao BWANA

Aliyeapa ingawa kwa hasara yake,

Hayabadili maneno yake.

5 Eze 18:8,9 Asiyetoa fedha yake apate kula riba,

Asiyepokea rushwa amwangamize asiye na hatia.

Mtu atendaye mambo hayo

Hataondoshwa milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help