Zaburi 12 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Ombi la msaada wakati wa dhikiKwa mwimbishaji: kwa kufuata Sheminithi. Zaburi ya Daudi.

1 Isa 57:1 Tuokoe, ee BWANA, maana hamna tena amchaye Mungu

Maana waaminifu wametoweka katika wanadamu.

2Husemezana yasiyofaa kila mtu na mwenziwe,

Wenye midomo ya kujipendekeza;

Husemezana kwa mioyo ya unafiki;

3BWANA ataikata midomo yote ya kujipendekeza,

Na ulimi unenao maneno ya kiburi;

4Waliosema, Kwa ndimi zetu tutashinda;

Midomo yetu ni yetu wenyewe,

Ni nani aliye bwana juu yetu?

5 Kut 3:7,8 Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge,

Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji,

Sasa nitasimama, asema BWANA,

Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.

6 2 Sam 22:31; Zab 18:30; Mit 30:5 Maneno ya BWANA ni maneno safi,

Ni fedha iliyojaribiwa kalibuni juu ya nchi;

Iliyosafishwa mara saba.

7Wewe, BWANA, ndiwe utakayetuhifadhi,

Utatulinda na kizazi hiki milele.

8Wasio haki hutembea pande zote,

Huku ufisadi ukitukuka kati ya wanadamu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help