Zaburi 114 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Maajabu ya Mungu wakati wa kutoka Misri

1 Kut 12:51 Haleluya.

Israeli alipotoka Misri,

Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.

2Yuda ilikuwa patakatifu pake,

Israeli milki yake.

3 Kut 14:21; Yos 3:16 Bahari iliona ikakimbia,

Yordani ilirudishwa nyuma.

4 Zab 29:6; 68:16; Hab 3:6 Milima iliruka kama kondoo dume,

Vilima kama wana-kondoo.

5Ee bahari, una nini, hata ukimbie?

Yordani, ndio urudi nyuma?

6Enyi milima, ndio mruke kama kondoo dume?

Enyi vilima, kama wana-kondoo?

7Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana,

Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.

8 Kut 17:1-7; Hes 20:2-13; Zab 107:35 Augeuzaye mwamba kuwa ziwa la maji,

Jiwe gumu kuwa chemchemi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help