Isaya 12 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Kushukuru na kusifu

1Katika siku ile utasema:

“Nitakusifu wewe, Ee Mwenyezi Mungu.

Ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imegeukia mbali

nawe umenifariji.

2Hakika Mungu ni wokovu wangu;

nitamtumaini wala sitaogopa.

Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu,

ni nguvu zangu na wimbo wangu;

amekuwa wokovu wangu.”

3Kwa furaha mtachota maji

kutoka visima vya wokovu.

4Katika siku hiyo mtasema:

“Mshukuruni Mwenyezi Mungu, mliitie jina lake;

julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

5Mwimbieni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ametenda mambo makuu,

hili na lijulikane duniani kote.

6Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,

kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help