Zaburi 54 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 54Kuomba ulinzi wa Mwenyezi Mungu kutokana na aduiKwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Wakati Wazifu walimwendea Sauli na kumjulisha, “Je, Daudi hajifichi miongoni mwetu?”

1Ee Mungu uniokoe kwa jina lako,

unifanyie hukumu kwa uwezo wako.

2Ee Mungu, sikia maombi yangu,

usikilize maneno ya kinywa changu.

3Wageni wananishambulia,

watu wakatili wanayatafuta maisha yangu,

watu wasiomjali Mungu.

4Hakika Mungu ni msaada wangu,

Bwana ndiye anayenitegemeza.

5Mabaya na yawarudie wale wanaonisingizia,

kwa uaminifu wako uwaangamize.

6Nitakutolea dhabihu za hiari;

Ee Mwenyezi Mungu, nitalisifu jina lako

kwa kuwa ni vyema.

7Kwa maana ameniokoa katika shida zangu zote,

na macho yangu yamewatazama adui zangu kwa ushindi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help