Zaburi 15 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 15Kitu Mwenyezi Mungu anachotakaZaburi ya Daudi.

1Mwenyezi Mungu, ni nani awezaye kukaa

katika Hekalu lako?

Nani awezaye kuishi

katika mlima wako mtakatifu?

2Ni yule aendaye pasipo mawaa,

atendaye yaliyo haki,

asemaye kweli toka moyoni mwake,

3na hana masingizio ulimini mwake,

asiyemtenda jirani yake vibaya,

na asiyemsingizia mwenzake,

4ambaye humdharau mtu mbaya,

lakini huwaheshimu wale wamwogopao Mwenyezi Mungu,

yule atunzaye kiapo chake

hata kama anaumia.

5Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,

na hapokei rushwa dhidi ya mtu asiye na hatia.

Mtu afanyaye haya

kamwe hatatikisika.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help