Zaburi 70 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 70Kuomba msaada(Zaburi 40:13-17)Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Maombi.

1Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa;

Ee Mwenyezi Mungu, njoo hima unisaidie.

2Wale wanaotafuta kuniua,

waaibishwe na kufadhaishwa;

wote wanaotamani kuangamizwa kwangu,

warudishwe nyuma kwa aibu.

3Wale wanaoniambia, “Aha! Aha!”

na warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

4Lakini wote wanaokutafuta

washangilie na kukufurahia,

wale wanaoupenda wokovu wako siku zote waseme,

“Mwenyezi Mungu ni mkuu!”

5Lakini mimi bado ni maskini na mhitaji;

Ee Mungu, unijie haraka.

Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu;

Ee Mwenyezi Mungu, usikawie.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help