Zaburi 13 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 13Sala ya kuomba msaadaKwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1Hadi lini, Ee Mwenyezi Mungu? Je, utanisahau milele?

Utanificha uso wako hadi lini?

2Nitapambana na mawazo yangu hadi lini,

na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?

Adui zangu watanishinda hadi lini?

3Nitazame, unijibu, Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wangu.

Yatie nuru macho yangu,

ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.

4Adui yangu atasema, “Nimemshinda,”

nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.

5Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;

moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.

6Nitamwimbia Mwenyezi Mungu,

kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help