1Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:
2“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5Ikiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
6sembuse mtu ambaye ni funza:
mwanadamu ambaye ni buu tu!”
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.