Zaburi 61 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 61Kuomba ulinziKwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za uimbaji. Zaburi ya Daudi.

1Ee Mungu, sikia kilio changu,

usikilize maombi yangu.

2Kutoka miisho ya dunia ninakuita,

ninakuita huku moyo wangu unadhoofika;

uniongoze kwenye mwamba

ulio juu kuniliko.

3Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu,

ngome imara dhidi ya adui.

4Natamani kukaa kwenye hema lako milele,

na kukimbilia chini ya uvuli wa mabawa yako.

5Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu,

umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.

6Mwongezee mfalme siku za maisha yake,

miaka yake kwa vizazi vingi.

7Mtawaze mbele za Mungu milele;

amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.

8Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako

na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help