Zaburi 1 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Kitabu cha Kwanza(Zaburi 1–41)Zaburi 1Furaha ya kweli

1Heri mtu yule ambaye haendi

katika shauri la watu waovu,

wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,

au kuketi katika baraza la wenye mizaha.

2Bali huifurahia Torati ya Mwenyezi Mungu,

naye huitafakari hiyo Torati usiku na mchana.

3Mtu huyo ni kama mti uliopandwa

kando ya vijito vya maji,

ambao huzaa matunda kwa majira yake

na majani yake hayanyauki.

Lolote afanyalo hufanikiwa.

Huzuni ya waovu

4Sivyo walivyo waovu!

Wao ni kama makapi

yanayopeperushwa na upepo.

5Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,

wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.

6Kwa maana Mwenyezi Mungu huziangalia njia za mwenye haki,

bali njia za waovu zitaangamia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help