Zaburi 20 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 20Maombi kwa ajili ya ushindiKwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1Mwenyezi Mungu na akujibu unapokuwa katika dhiki,

jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.

2Na akutumie msaada kutoka patakatifu

na akupatie msaada kutoka Sayuni.

3Na azikumbuke dhabihu zako zote,

na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.

4Na akujalie haja ya moyo wako,

na aifanikishe mipango yako yote.

5Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda,

tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu.

Mwenyezi Mungu na akupe haja zako zote.

6Sasa nafahamu kuwa Mwenyezi Mungu

humwokoa mpakwa mafuta wake,

humjibu kutoka mbingu yake takatifu

kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.

7Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi,

bali sisi tutalitumainia jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wetu.

8Wao wameshushwa chini na kuanguka,

bali sisi tunainuka na kusimama imara.

9Ee Mwenyezi Mungu, mwokoe mfalme!

Tujibu tunapokuita!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help