Zaburi 65 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 65Kusifu na kushukuruKwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo.

1Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni;

kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.

2Ewe usikiaye maombi,

watu wote watakuja kwako wewe.

3Tulipokuwa tumefunikwa kabisa na dhambi,

wewe ulisamehe makosa yetu.

4Heri wale uliowachagua

na kuwaleta karibu ili waishi katika nyua zako!

Tunashibishwa kwa mema ya nyumba yako,

mema ya Hekalu lako takatifu.

5Unatujibu kwa matendo ya kushangaza ya haki,

Ee Mungu Mwokozi wetu,

tumaini la miisho yote ya duniani

na la bahari zilizo mbali sana,

6uliyeumba milima kwa uwezo wako,

ukiwa umejivika nguvu,

7uliyenyamazisha dhoruba za bahari,

ngurumo za mawimbi yake,

na ghasia za mataifa.

8Wale wanaoishi mbali sana

wanaogopa maajabu yako,

kule asubuhi ipambazukiapo

na kule jioni inakofifilia

umeziita nyimbo za furaha.

9Waitunza nchi na kuinyeshea,

waitajirisha kwa wingi.

Vijito vya Mungu vimejaa maji

ili kuwapa watu nafaka,

kwa maana wewe umeviamuru.

10Umeilowesha mifereji yake

na kusawazisha kingo zake;

umeilainisha kwa manyunyu

na kuibariki mimea yake.

11Umeuvika mwaka taji la baraka,

magari yako yanafurika kwa wingi.

12Mbuga za majani za jangwani umezineemesha;

vilima vimevikwa furaha.

13Malisho yamejaa makundi ya wanyama,

na mabonde yamepambwa kwa mavuno;

vyote vinashangilia kwa furaha na kuimba.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help