Zaburi 113 - Kiswahili Contemporary Scriptures 2024

Zaburi 113Kumsifu Mwenyezi Mungu kwa wema wake

1Msifuni Mwenyezi Mungu.

Enyi watumishi wa Mwenyezi Mungu msifuni,

lisifuni jina la Mwenyezi Mungu.

2Jina la Mwenyezi Mungu na lisifiwe,

sasa na hata milele.

3Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,

jina la Mwenyezi Mungu linapaswa kusifiwa.

4Mwenyezi Mungu ametukuka juu ya mataifa yote,

utukufu wake juu ya mbingu.

5Ni nani aliye kama Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,

Yule aliyeketi kwenye kiti cha enzi huko juu,

6ambaye huinama atazame chini

aone mbingu na nchi?

7Huwainua maskini kutoka mavumbini,

na kuwanyanyua wahitaji

kutoka lundo la majivu,

8huwaketisha pamoja na wakuu,

pamoja na wakuu wa watu wake.

9Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,

akiwa mama watoto mwenye furaha.

Msifuni Mwenyezi Mungu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help