1Tazama jinsi ilivyo vyema na kupendeza
ndugu wanapoishi pamoja katika umoja!
2Ni kama mafuta ya thamani yaliyomiminwa kichwani,
yakitiririka kwenye ndevu,
yakitiririka kwenye ndevu za Haruni,
hadi kwenye upindo wa mavazi yake.
3Ni kama umande wa Hermoni
ukianguka juu ya Mlima Sayuni.
Kwa maana huko ndiko Bwana alikoamuru baraka yake,
naam, uzima hata milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.