Zaburi 29 - Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) 2025

Zaburi 29Sauti ya Bwana

wakati wa dhorubaZaburi ya Daudi.

1Mpeni Bwana, enyi mashujaa,

mpeni Bwana utukufu na nguvu.

2Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;

mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.

3Sauti ya Bwana iko juu ya maji;

Mungu wa utukufu hupiga radi,

Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.

4Sauti ya Bwana ina nguvu;

sauti ya Bwana ni tukufu.

5Sauti ya Bwana huvunja mierezi;

Bwana huvunja vipande vipande

mierezi ya Lebanoni.

6Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,

Sirioni urukaruke kama mwana nyati.

7Sauti ya Bwana hupiga

kwa miali ya radi.

8Sauti ya Bwana hutikisa jangwa;

Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.

9Sauti ya Bwana huzalisha ayala,

na huuacha msitu wazi.

Hekaluni mwake wote wasema,

“Utukufu!”

10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;

Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.

11 Bwana huwapa watu wake nguvu;

Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help