Ayubu 23 - Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) 2025

Hotuba ya nane ya AyubuAyubu anajibu: Nalalamika kwa uchungu

1Ndipo Ayubu akajibu:

2“Hata leo malalamiko yangu ni ya uchungu;

mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.

3Laiti ningefahamu mahali pa kumwona;

laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!

4Ningeleta kesi yangu mbele zake,

na kukijaza kinywa changu na hoja.

5Ningejua kwamba angenijibu nini,

na kuelewa lile angeniambia.

6Je, angenipinga kwa nguvu nyingi?

La, hangenigandamiza.

7Hapo mtu mwadilifu angeleta kesi yake mbele zake,

nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.

8“Lakini nikienda mashariki, hayupo;

nikienda magharibi, simpati.

9Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni;

akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.

10Lakini anaijua njia niiendeayo;

akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

11Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu;

nimeishika njia yake bila kukengeuka.

12Sijaziacha amri zilizotoka mdomoni mwake;

nimeyathamini maneno ya kinywa chake

kuliko chakula changu cha kila siku.

13“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga?

Yeye hufanya lolote atakalo.

14Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu,

na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.

15Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake;

nifikiriapo haya yote ninamwogopa.

16Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia;

yeye Mwenyezi amenitia hofu.

17Hata hivyo sijanyamazishwa na giza,

wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help