Zaburi 130 - Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) 2025

Zaburi 130Kumngojea Bwana

Wimbo wa kwenda juu.

1Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.

2Ee Bwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

Ee Bwana, ni nani angeweza kusimama?

4Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7Ee Israeli, mtumaini Bwana,

maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka dhambi zao zote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help