Zaburi 122 - Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) 2025

Zaburi 122Sifa kwa YerusalemuWimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1Nilishangilia pamoja na wale walioniambia,

“Twende nyumbani mwa Bwana.”

2Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama

malangoni mwako.

3Yerusalemu imejengwa vyema kama mji

ulioshikamana pamoja.

4Huko ndiko makabila hukwea,

makabila ya Bwana,

kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo

waliopewa Israeli.

5Huko viti vya hukumu hukaa,

viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.

6Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu:

“Wote wanaokupenda na wawe salama.

7Amani na iwe ndani ya kuta zako,

na usalama ndani ya ngome zako.”

8Kwa ajili ya ndugu na rafiki zangu,

nitasema, “Amani iwe ndani yako.”

9Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu,

nitatafuta mafanikio yako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help