1Nayainua macho yangu natazama milima:
msaada wangu utatoka wapi?
2Msaada wangu hutoka kwa Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
3Hatauacha mguu wako uteleze,
yeye akulindaye hatasinzia,
4hakika, yeye alindaye Israeli
hatasinzia wala hatalala usingizi.
5 Bwana anakulinda,
Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,
6jua halitakudhuru mchana,
wala mwezi wakati wa usiku.
7 Bwana atakukinga na madhara yote,
atayalinda maisha yako,
8 Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka,
tangu sasa na hata milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.