1Kama Bwana hangekuwa upande wetu;
Israeli na aseme sasa:
2kama Bwana hangekuwa upande wetu,
watu walipotushambulia,
3hasira yao ilipowaka dhidi yetu,
wangetumeza tukiwa hai,
4mafuriko yangegharikisha,
maji mengi yangetufunika,
5maji yaendayo kasi
yangetuchukua.
6Ahimidiwe Bwana,
ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7Tumeponyoka kama ndege
kutoka mtego wa mwindaji;
mtego umevunjika,
nasi tumeokoka.
8Msaada wetu ni katika jina la Bwana,
Muumba wa mbingu na dunia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.