1 Bwana anatawala, amejivika utukufu;
Bwana amejivika utukufu
tena amejivika nguvu.
Dunia imewekwa imara,
haitaondoshwa.
2Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani;
wewe umekuwa tangu milele.
3Bahari zimepaza, Ee Bwana,
bahari zimepaza sauti zake;
bahari zimepaza sauti za mawimbi yake.
4Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu,
ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari:
Bwana aishiye juu sana ni mkuu.
5Ee Bwana, sheria zako ni imara;
utakatifu umepamba nyumba yako
pasipo mwisho.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.