Zaburi 99 - Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) 2025

Zaburi 99Mungu Mfalme mtakatifu

1 Bwana anatawala,

mataifa na yatetemeke;

anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi,

dunia na itikisike.

2 Bwana ni mkuu katika Sayuni;

ametukuzwa juu ya mataifa yote.

3Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa:

yeye ni mtakatifu!

4Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki,

wewe umethibitisha adili;

katika Yakobo umefanya

yaliyo haki na sawa.

5Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake;

yeye ni mtakatifu.

6Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,

Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake;

walimwita Bwana,

naye aliwajibu.

7Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu;

walizishika sheria zake na amri alizowapa.

8Ee Bwana, wetu,

ndiwe uliyewajibu,

kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,

ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

9Mtukuzeni Bwana Mungu wetu,

mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu,

kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help