1 Wafalme Utangulizi - Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) 2025
UtanguliziKatika maandiko ya Kiebrania, vitabu vya 1 Wafalme na 2 Wafalme vilikuwa kitabu kimoja kilichoitwa “Wafalme” katika mapokeo ya Kiyahudi. Huku kutenganishwa kwa vitabu hivi kulifanywa na watafsiri wa Agano la Kale la Kiyunani linaloitwa “Septuagint” na vikatambulishwa kama “Kitabu cha Tatu na cha Nne cha Ufalme.” Vitabu vya Samweli na Wafalme vinaelezea historia yote kuhusu ufalme wa Israeli, vile ulivyoinuka wakati wa Samweli, na vile ulivyoanguka mikononi mwa Wababeli.MwandishiMwandishi wa kitabu hiki hajulikani, lakini mapokeo ya Kiyahudi yanasema mwandishi ni nabii Yeremia, au kikundi cha manabii.KusudiKulinganisha maisha ya wale waliomwishia Mungu na wale waliokataa kumwishia Mungu, kupitia historia ya wafalme wa Israeli na Yuda.MahaliKatika nchi ya Israeli.TareheWakati kitabu hiki kiliandikwa haujulikani.Wahusika WakuuDaudi, Sulemani, Rehoboamu, Yeroboamu, Eliya, Ahabu na Yezebeli.Wazo KuuKugawanyika kwa Israeli kuwa falme mbili: Ufalme wa Kaskazini uliojulikana kama Israeli, ambao ulikuwa na makabila kumi, na Ufalme wa Kusini uliojulikana kama Yuda, ambao ulikuwa na makabila mawili.Mambo MuhimuKifo cha Daudi, utawala wa Sulemani, kujengwa kwa Hekalu, kugawanyika kwa ufalme, na huduma ya Eliya.YaliyomoUtawala wa Sulemani (1:1–11:43)Rehoboamu na Yeroboamu (12:1–14:31)Wafalme wa Israeli na Yuda (15:1–16:34)Eliya na Ahabu (17:1–19:21)Utawala wa Ahabu na Yezebeli (20:1–22:53).