1Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
2Mt 17:20; 7:22; 21:21; Mk 11:23Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi.
3Mt 6:2Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.
4Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;
5Zek 8:17; Flp 2:4haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;
6Rum 12:9haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;
7Mit 10:12; 1 Kor 9:12; Rum 15:1huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.
81 Pet 4:8Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.
9Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu;
10lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika.
11Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto.
122 Kor 5:7; Yak 1:23Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana.
131 The 1:3; 1 Yoh 4:16Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.