Zab 15 - Swahili Union Version Bible

Nani Atakaa katika Patakatifu pa Mungu?Zaburi ya Daudi.

1 Zab 2:5 BWANA, ni nani atakayekaa

Katika hema yako?

Ni nani atakayefanya maskani yake

Katika kilima chako kitakatifu?

2 Zab 84:11; Isa 33:15,16 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu,

Na kutenda haki.

Asemaye kweli kwa moyo wake,

3Asiyesingizia kwa ulimi wake.

Wala hakumtenda mwenziwe mabaya,

Wala hakumsengenya jirani yake.

4 Yos 9:18-20 Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa,

Bali huwaheshimu wamchao BWANA

Ingawa ameapa kwa hasara yake,

Hayabadili maneno yake.

5 Eze 18:8,9 Hakutoa fedha yake apate kula riba,

Hakutwaa rushwa amwangamize asiye na hatia.

Mtu atendaye mambo hayo

Hataondoshwa milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help