Zab 99 - Swahili Union Version Bible

Sifa kwa Utukufu wa Mungu

1 Kut 25:22 BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;

Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.

2BWANA katika Sayuni ni mkuu,

Naye ametukuka juu ya mataifa yote.

3 Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8 Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa;

Ndiye mtakatifu.

4 Kum 32:3,4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Mwa 18:25 Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu;

Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili;

Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.

5 1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;

Sujuduni penye kiti cha miguu yake;

Ndiye mtakatifu.

6Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake,

Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake,

Walipomwita Bwana aliwaitikia;

7 Kut 19:9; Kut 33:9; Hes 12:5 Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao.

Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.

8 Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20 Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;

Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe

Ingawa uliwapatiliza matendo yao.

9Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;

Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;

Maana BWANA, Mungu wetu, ndiye mtakatifu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help