Zab 120 - Swahili Union Version Bible

Sala ya UkomboziWimbo wa Kupanda Mlima.

1Katika shida yangu nalimlilia BWANA

Naye akaniitikia.

2Ee BWANA, uiponye nafsi yangu

Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.

3Akupe nini, akuzidishie nini,

Ewe ulimi wenye hila?

4Mishale ya mtu hodari iliyochongoka,

Pamoja na makaa ya mretemu.

5 Mwa 10:2; 1 Sam 25:1; Yer 49:28 Ole wangu mimi!

Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki;

Na kufanya maskani yangu

Katikati ya hema za Kedari.

6Nafsi yangu imekaa siku nyingi,

Pamoja naye aichukiaye amani.

7Mimi ni wa amani;

Bali ninenapo, wao huelekea vita.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help