Zab 76 - Swahili Union Version Bible

Mungu wa Waisraeli - Mungu MkuuKwa mwimbishaji: kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo.

1Katika Yuda Mungu amejulikana,

Katika Israeli jina lake ni kuu.

2Kibanda chake pia kiko Salemu,

Na maskani yake iko Sayuni.

3 Zab 46:9; Eze 39:9 Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta,

Ngao, na upanga, na zana za vita.

4 Eze 38:12 Wewe U mwenye fahari na adhama,

Toka milima ya mateka.

5 Isa 46:12; Zab 13:3; Yer 51:39 Wametekwa wenye moyo thabiti;

Wamelala usingizi;

Wala hawakuiona mikono yao

Watu wote walio hodari.

6 Kut 15:1; Nah 2:13; Zek 12:4 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo,

Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.

7 Ayu 41:10; Nah 1:6 Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe;

Naye ni nani awezaye kusimama ufanyapo hasira?

8Toka mbinguni ulitangaza hukumu;

Nchi iliogopa, ikakaa kimya.

9Mungu aliposimama ili kuhukumu

Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.

10 Kut 9:16 Maana hasira ya binadamu itakusifu,

Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.

11 Mhu 5:4; Zab 68:29 Wekeni nadhiri, mkaziondoe

Kwa BWANA, Mungu wenu.

Wote wanaomzunguka wamletee hedaya,

Yeye astahiliye kuogopwa.

12 Zab 68:35 Yeye huzikata roho za wakuu;

Na kuwatisha wafalme wa dunia.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help