Isa 62 - Swahili Union Version Bible

Uthibitisho wa Wokovu wa Sayuni

1Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo.

2 na nchi yako Beula; kwa kuwa BWANA anakufurahia, na nchi yako itaolewa.

5Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

6 Wim 3:3; Isa 52:8; Eze 3:17; Ebr 13:17 Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, Ee Yerusalemu; hawatanyamaza mchana wala usiku; ninyi wenye kumkumbusha BWANA, msiwe na kimya;

7Isa 61:11; Sef 3:20wala msimwache akae kimya, mpaka atakapoufanya imara Yerusalemu, na kuufanya kuwa sifa duniani.

8Kum 28:31; Yer 5:17BWANA ameapa kwa mkono wake wa kuume, na kwa mkono wa nguvu zake, Hakika sitawapa adui zako nafaka yako tena kuwa chakula chao; wala wageni hawatakunywa divai yako, uliyoifanyia kazi.

9Kum 12:12Lakini walioivuna, ndio watakaoila, na kumhimidi BWANA; na walioichuma, ndio watakaoinywa, ndani ya nyua za patakatifu pangu.

10Piteni, piteni, katika malango;

Itengenezeni njia ya watu;

Tutieni, tutieni barabara; toeni mawe yake;

Twekeni bendera kwa ajili ya kabila za watu.

11 Zek 9:9; Mt 21:5; Yn 12:15; Isa 40:10; 49:4; Ufu 22:12 Tazama, BWANA ametangaza habari mpaka mwisho wa dunia,

Mwambieni binti Sayuni,

Tazama, wokovu wako unakuja;

Tazama, thawabu yake i pamoja naye,

Na malipo yake yako mbele zake.

12Nao watawaita, Watu watakatifu,

Waliokombolewa na BWANA;

Nawe utaitwa, Aliyetafutwa,

Mji usioachwa.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help