Zab 111 - Swahili Union Version Bible

Sifa kwa Maajabu ya Mungu

1Haleluya.

Nitamshukuru BWANA kwa moyo wangu wote,

Barazani pa wanyofu wa moyo na katika mkutano.

2 Ayu 38:1 Matendo ya BWANA ni makuu,

Yafikiriwa sana na wapendezwao nayo.

3Kazi yake ni heshima na adhama,

Na haki yake yakaa milele.

4Amefanya ukumbusho wa matendo yake ya ajabu;

BWANA ni mwenye fadhili na rehema.

5Amewapa wamchao chakula;

Atalikumbuka agano lake milele.

6Amewajulisha watu wake uwezo wa matendo yake,

Kwa kuwapa urithi wa mataifa.

7 Zab 19:7 Matendo ya mikono yake ni kweli na hukumu,

Maagizo yake yote ni amini,

8 Ufu 15:3 Yamethibitika milele na milele,

Yamefanywa katika kweli na adili.

9Amewapelekea watu wake ukombozi,

Ameamuru agano lake liwe la milele,

Jina lake ni takatifu la kuogopwa.

10 Kum 4:6; Ayu 28:28; Mit 1:7; 9:10; Mhu 12:3 Kumcha BWANA ndio mwanzo wa hekima,

Wote wafanyao hayo wana akili njema,

Sifa zake zakaa milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help