1Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,
Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
2 Zab 6:2-4 Ee BWANA, Mungu wangu,
Nalikulilia ukaniponya.
3 Zab 40:1,2 Umeniinua nafsi yangu,
Ee BWANA, kutoka kuzimu.
Umenihuisha na kunitoa
Miongoni mwao washukao shimoni.
4Mwimbieni BWANA zaburi,
Enyi watauwa wake.
Na kufanya shukrani.
Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.
5 Zab 16:11; Ufu 22:17 Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,
Katika radhi yake mna uhai.
Huenda kilio huja kukaa usiku,
Lakini asubuhi huwa furaha.
6 Ayu 29:18 Nami nilipofanikiwa nalisema,
Sitaondoshwa milele.
7 Zab 104:29 BWANA, kwa radhi yako
Wewe uliuimarisha mlima wangu.
Uliuficha uso wako,
Nami nikafadhaika.
8Ee BWANA, nalikulilia Wewe,
Naam, kwa BWANA naliomba dua.
9 Zab 115:17 Mna faida gani katika damu yangu
Nishukapo shimoni?
Mavumbi yatakusifu?
Yataitangaza kweli yako?
10 Zab 4:1 Ee BWANA, usikie, unirehemu,
BWANA, uwe msaidizi wangu.
11 2 Sam 6:14 Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;
Ulinivua gunia, ukanivika furaha.
12Ili utukufu wangu ukusifu,
Wala usinyamaze.
Ee BWANA, Mungu wangu,
Nitakushukuru milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.