1Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo;
Umenifanyizia nafasi wakati wa shida;
Unifadhili na kuisikia sala yangu.
2Enyi wanadamu, hata lini utukufu wangu utafedheheka?
Je! Mtapenda ubatili na kutafuta uongo?
3 Kut 33:16; 2 Pet 2:9 Bali jueni ya kuwa BWANA amejiteulia mtauwa;
BWANA atasikia nimwitapo.
4 Efe 4:26; Mit 3:7 Mwe na hofu wala msitende dhambi,
Tafakarini vitandani mwenu na kutulia.
5 Kum 33:19; Zab 37:3 Toeni dhabihu za haki,
Na kumtumaini BWANA.
6 Zab 80:3 Wengi husema, Nani atakayetuonyesha mema?
BWANA, utuinulie nuru ya uso wako.
7Umenitia furaha moyoni mwangu,
Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.
8 Law 26:5; Kum 12:10; Yn 14:27; Flp 4:7 Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara,
Maana Wewe, BWANA, peke yako,
Ndiwe unijaliaye kukaa salama.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.