Zab 127 - Swahili Union Version Bible

Baraka za Mungu NyumbaniWimbo wa kupanda mlima.

1BWANA asipoijenga nyumba

Waijengao wafanya kazi bure.

BWANA asipoulinda mji

Yeye aulindaye akesha bure.

2 Mwa 3:17 Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema,

Na kukawia kwenda kulala,

Na kula chakula cha taabu;

Yeye humpa mpenzi wake usingizi.

3 Mwa 33:5; Kum 28:4 Tazama, wana ndio urithi wa BWANA,

Uzao wa tumbo ni thawabu.

4Kama mishale mkononi mwa shujaa,

Ndivyo walivyo wana wa ujanani.

5Heri mtu yule

Aliyelijaza podo lake hivyo.

Naam, hawataona aibu

Wanaposema na adui langoni.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help