1Sala ya nabii Habakuki.
2Ee BWANA, nimesikia habari zako, nami naogopa;
Ee BWANA, fufua kazi yako katikati ya miaka;
Katikati ya miaka tangaza habari yake;
Katika ghadhabu kumbuka rehema.
3Mungu alikuja kutoka Temani,
Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani.
Utukufu wake ukazifunika mbingu,
Nayo dunia ikajaa sifa yake.
4Mwangaza wake ulikuwa kama nuru;
Alikuwa na mishale ya nuru ubavuni pake;
Ndipo ulipofichwa uweza wake.
5Mbele zake ilikwenda tauni,
Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake.
6 wako;
Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu,
Ukiuweka wazi msingi hata mwambani.
14Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe;
Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya;
Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri.
15Ukaikanyaga bahari kwa farasi wako,
Chungu ya maji yenye nguvu.
16Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka,
Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile;
Ubovu ukaingia mifupani mwangu,
Nikatetemeka katika mahali pangu;
Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki,
Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu.
Imani na shangwe katika shida17
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.