Zaburi 61 - Swahili Revised Union Version DC

Hakikisho la ulinzi wa MunguKwa mwimbishaji: kwa ala za nyuzi za muziki. Ya Daudi.

1Ee Mungu, ukisikie kilio changu,

Uyasikilize maombi yangu.

2 1 Tim 2:8 Toka mwisho wa nchi nitakulilia ninapozimia moyo,

Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.

3 Mit 18:10 Kwa maana ulikuwa kimbilio langu,

Ngome yenye nguvu adui asinipate.

4 Zab 15:1; 23:6; Ufu 3:12 Nitakaa katika hema yako milele,

Na kupata kimbilio chini ya mbawa zako.

5 1 Kor 3:21-23 Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu.

Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.

6Utaziongeza siku za mfalme,

Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.

7 Zab 41:12; Lk 1:32 Atakaa mbele za Mungu milele,

Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.

8 Zab 56:12 Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima,

Ili niondoe nadhiri zangu kila siku.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help