Ayubu 26 - Swahili Revised Union Version DC

Ayubu ajibu: Ukuu wa Mungu hauchunguziki

1Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,

2 Mit 25:11 Jinsi ulivyomsaidia huyo asiye na uwezo!

Jinsi ulivyouokoa mkono usio na nguvu!

3 1 Kor 2:4 Jinsi ulivyomshauri huyo asiye na hekima!

Na kutangaza ujuzi wa kweli kwa wingi!

4Je! Umetamka maneno kwa nani?

Kisha ni roho ya nani iliyotoka kwako?

5Hao waliokufa watetemesha

Chini ya maji na hao wakaamo humo.

6 Zab 139:8; Mit 15:11; Isa 14:9; Amo 9:2; Ebr 4:13 Kaburi li wazi mbele yake,

Uharibifu nao hauna kifuniko.

7 Zab 24:1,2 Yeye hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu,

Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu.

8 Mit 30:4 Huyafunga maji ndani ya mawingu yake mazito;

Na hilo wingu halipasuki chini yake.

9Husitiri uso wa kiti chake cha enzi,

Na kulitandaza wingu lake juu yake.

10 Yer 5:22 Amepiga duara kuwa ni mpaka juu ya uso wa maji,

Hata hapo mwanga na giza vinapopakana.

11Nguzo za mbingu zatetemeka,

Na kustaajabu kwa kukemea kwake.

12 Kut 14:21; Isa 51:15; Zab 29:10; 74:13 Huichafua bahari kwa uwezo wake,

Na kumtema Rahabu kwa akili zake.

13 Zab 33:6 Hizo mbingu hupambwa kwa roho yake;

Mkono wake umemchoma nyoka aendaye mbio.

14Tazama, hivi ni viunga tu vya njia zake;

Na jinsi yalivyo madogo manong'ono tusikiayo katika habari zake!

Lakini ngurumo za uweza wake ni nani awezaye kuzielewa?

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help