Zaburi 128 - Swahili Revised Union Version DC

Nyumba ya mwumini yenye furahaWimbo wa kupanda mlima.

1Heri kila mtu amchaye BWANA,

Aendaye katika njia yake.

2 Isa 3:10 Taabu ya mikono yako hakika utaila;

Utakuwa heri, na kwako kwema.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,

Katika nyumba yako.

Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni

Wakiizunguka meza yako.

4Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.

5 Zab 134:3 BWANA akubariki toka Sayuni;

Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;

6 Mwa 50:23 Naam, ukawaone wana wa wanao.

Amani ikae na Israeli.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help