Zaburi 16 - Swahili Revised Union Version DC

Wimbo wa imani na usalama kwa MunguWimbo wa Daudi.

1 Zab 25:20 Mungu, unihifadhi mimi,

Kwa maana nakukimbilia Wewe.

2Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;

Sina wema ila utokao kwako.

3Nao watakatifu waliopo duniani, ndio Walio bora,

Hao ndio niliopendezwa nao.

4Huzuni zao zitaongezeka

Wambadilio Mungu kwa mwingine;

Sitazimimina sadaka zao za damu,

Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.

5BWANA ndiye fungu la posho langu,

Na la kikombe changu;

Wewe unayaamua maisha yangu.

6Mipaka yangu imeangukia mahali pema,

Naam, nimepata urithi mzuri.

7Nitamhimidi BWANA aniongozaye,

Wakati wa usiku pia moyo wangu hunishauri.

8 Mdo 2:25-28 Nimemweka BWANA mbele yangu daima,

Kwa kuwa yuko kuliani mwangu, sitaondoshwa.

9Kwa hiyo moyo wangu unafurahi,

Nayo nafsi yangu inashangilia,

Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini.

10 Mdo 13:35; Zab 49:15; Mdo 2:27; Dan 9:24; Lk 1:35 Maana hutaitupa kuzimu nafsi yangu,

Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.

11 Mdo 2:28 Utanijulisha njia ya uzima;

Mbele za uso wako kuna furaha tele;

Na katika mkono wako wa kulia

Mna mema ya milele.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help