Zaburi 148 - Swahili Revised Union Version DC

Sifa kwa utukufu mkuu wa Mungu

1Haleluya.

Msifuni BWANA kutoka mbinguni;

Msifuni katika mahali palipo juu.

2 Dan 7:10; Ebr 1:7 Msifuni, enyi malaika wake wote;

Msifuni, majeshi yake yote.

3Msifuni, jua na mwezi;

Msifuni, nyota zote zenye mwanga.

4 1 Fal 8:27 Msifuni, enyi mbingu za mbingu,

Nanyi maji mlioko juu ya mbingu.

5 Ebr 11:3 Na vilisifu jina la BWANA,

Kwa maana aliamuru, vikaumbwa.

6 Yer 33:25 Amevithibitisha hata milele na milele,

Ametoa amri wala haitapita.

7 Isa 43:20 Msifuni BWANA kutoka nchi,

Enyi nyangumi na vilindi vyote.

8Moto na mvua ya mawe, theluji na mvuke,

Upepo wa dhoruba utimizao neno lake.

9 Isa 49:13 Milima na vilima vyote,

Miti yenye matunda na mierezi yote.

10Hayawani, na wanyama wafugwao,

Vitambaavyo, na ndege wenye mbawa.

11 Mdo 17:28 Wafalme wa dunia, na watu wote,

Wakuu, na watawala wote wa dunia.

12Vijana wa kiume, na wanawali,

Wazee, na watoto;

13 Isa 6:3; Flp 2:9 Na walisifu jina la BWANA,

Maana jina lake peke yake limetukuka;

Adhama yake i juu ya nchi na mbingu.

14 Efe 2:17; 1 Pet 2:9 Naye amewainulia watu wake pembe,

Sifa za watauwa wake wote;

Wana wa Israeli, watu walio karibu naye.

Haleluya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help