1 1 Sam 22:9-10; 21:7 Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari?
Wema wa Mungu upo sikuzote.
2 Zab 50:19; Mit 12:18; Zab 59:7 Ulimi wako watunga madhara,
Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila.
3 Yer 9:4 Umependa mabaya kuliko mema,
Na uongo kuliko kusema kweli.
4Umependa maneno yote ya kupoteza watu,
Ewe ulimi wenye hila.
5 Mit 2:22 Lakini Mungu atakuharibu hata milele;
Atakuondolea mbali;
Atakunyakua hemani mwako;
Atakung'oa katika nchi ya walio hai.
6 Ayu 22:19; Zab 58:10 Nao wenye haki wataona;
Wataingiwa na hofu na kumcheka;
7 Ayu 31:24,25; Zab 49:6 Kumbe! Huyu ndiye mtu yule,
Asiyemfanya Mungu kuwa kimbilio lake.
Aliutumainia wingi wa mali zake,
Na kufanya mali kimbilio lake.
8 Zab 92:13 Bali mimi ni kama mzeituni
Umeao katika nyumba ya Mungu.
Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.
9 Zab 54:6 Nitakushukuru milele kwa maana umetenda;
Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema;
Mbele ya wacha Mungu wako.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.