Ayubu 33 - Swahili Revised Union Version DC

Elihu amkemea Ayubu

1 Ayu 13:6 Lakini, Ayubu, nakuomba usikilize hoja yangu,

Ukayasikilize maneno yangu yote.

2Tazama basi, nimefunua kinywa changu,

Ulimi wangu umenena kinywani mwangu.

3 1 The 1:3 Maneno yangu yatatamka uelekevu wa moyo wangu;

Na hayo niyajuayo midomo yangu itayanena kwa unyofu.

4 Mwa 2:7 Roho ya Mungu imeniumba,

Na pumzi za Mwenyezi hunipa uhai.

5Ikiwa unaweza, nijibu;

Yapange maneno yako sawasawa mbele yangu, usimame.

6 Ayu 9:32 Tazama, mimi ni mbele ya Mungu kama ulivyo wewe;

Mimi nami nilifinyangwa katika udongo.

7 Ayu 13:21 Tazama, utisho wangu hautakutia hofu wewe,

Wala sitakulemea kwa uzito.

8Hakika umenena masikioni mwangu,

Nami nimesikia sauti ya maneno yako, ukisema,

9 Ayu 10:7 Mimi ni safi, sina makosa;

Sina hatia, wala hapana uovu ndani yangu;

10 Ayu 13:24 Tazama, yuaona sababu za kufarakana nami,

Hunihesabu kuwa ni adui yake;

11 Ayu 13:27 Hunitia miguu yangu katika mkatale,

Na mapito yangu yote huyapeleleza.

12 Mhu 7:20 Tazama, nitakujibu, katika neno hili huna haki;

Kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.

13 Isa 45:9 Kwa nini unapingana naye, ukisema,

Hatajibu hata neno langu moja?

14Kwa kuwa Mungu hunena mara moja,

Naam, hata mara ya pili, ijapokuwa mtu hatambui.

15 Ayu 4:13 Katika ndoto, katika maono ya usiku,

Usingizi mzito uwajiapo watu,

Katika usingizi kitandani;

16Ndipo huyafunua masikio ya watu,

Na kuyatia mhuri mafundisho yao,

17Ili amwondoe mtu katika makusudio yake,

Na kumfichia mtu kiburi;

18Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni,

Na uhai wake usiangamie kwa upanga.

19 Kum 8:5; Zab 94:12,13 Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake,

Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake;

20Hata roho yake huchukia chakula,

Na nafsi yake huchukia nyama nzuri.

21 Zab 102:5 Nyama ya mwili wake huliwa, isionekane;

Na mifupa yake isiyoonekana yatokeza nje.

22Naam, nafsi yake inakaribia shimoni,

Na uhai wake unakaribia waangamizi.

23 2 Nya 36:15,16; Mal 2:7 Lakini akiwapo malaika pamoja naye,

Mpatanishi, mmoja katika elfu,

Ili kumwonesha binadamu hayo yampasayo;

24 Rum 3:24 Ndipo amwoneapo rehema, na kusema,

Mwokoe asishuke shimoni;

Mimi nimeuona ukombozi.

25Nyama ya mwili wake itakuwa laini kuliko ya mtoto;

Huzirudia siku za ujana wake;

26 2 Fal 20:2-5; Zab 6:1-9 Yeye humwomba Mungu, naye akamtakabalia;

Hata auone uso wake kwa furaha;

Naye humrejeshea mtu haki yake.

27Yeye huimba mbele ya watu, na kusema,

Mimi nimefanya dhambi, na kuyapotosha hayo yaliyoelekea,

Wala sikulipizwa jambo hilo;

28Yeye ameikomboa nafsi yangu isiende shimoni,

Na uhai wangu utautazama mwanga.

29Tazama, hayo yote ni Mungu anayeyafanya,

Mara mbili, naam, hata mara tatu, kwa mtu,

30 Zab 40:2; Zek 9:11 Ili kurudisha roho yake itoke shimoni,

Ili atiwe mwanga kwa mwanga wa walio hai.

31Angalia sana, Ee Ayubu, unisikilize;

Nyamaza, mimi nitasema.

32 2 Kor 1:24 Kama una neno la kusema, nijibu;

Nena, kwani nataka kukuhesabia kuwa na haki.

33 Zab 34:11 Kama sivyo, unisikilize mimi;

Nyamaza, nami nitakufunza hekima.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help