Zaburi 82 - Swahili Revised Union Version DC

Ombi la kupata hakiZaburi ya Asafu.

1 Mhu 5:8; Kut 21:6 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;

Katikati ya miungu anahukumu.

2 Kum 1:17; Zab 58:1,2 Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma,

Na kuzikubali nyuso za wabaya?

3Mfanyieni hukumu maskini na yatima;

Mtendeeni haki aliyeonewa, na fukara;

4Mwokoeni maskini na mhitaji;

Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.

5 Zab 11:3 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;

Misingi yote ya nchi imetikisika.

6 Ayu 21:32; Eze 31:14; Yn 10:34 Mimi nimesema, Ndinyi miungu,

Na wana wa Aliye Juu, enyi nyote.

7Lakini mtakufa kama wanadamu,

Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.

8 Zab 2:8; Ufu 11:15 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi,

Maana mataifa yote ni yako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help