1Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza,
Nitalihimidi jina lako milele na milele.
2Kila siku nitakuhimidi,
Nitalisifu jina lako milele na milele.
3BWANA ndiye mkuu mwenye kusifiwa sana,
Wala ukuu wake hauchunguziki.
4Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako,
Kitayatangaza matendo yako makuu.
5Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako,
Na matendo yako yote ya ajabu.
6Watu watayataja matendo yako ya kutisha,
Nami nitausimulia ukuu wako.
7Watasimulia juu ya ukuu wa wema wako mwingi.
Na wataiimba haki yako kwa sauti.
8
10
Na mamlaka yako ni ya vizazi vyote.
14BWANA huwategemeza wote waangukao,
Huwainua wote walioinama chini.
15Macho ya watu wote yakuelekea Wewe,
Nawe huwapa chakula chao wakati wake.
16Waufumbua mkono wako,
Wakishibisha kila kilicho hai matakwa yake.
17BWANA ni mwenye haki katika njia zake zote,
Na mwenye huruma katika matendo yake yote.
18 Zab 91:1; Isa 61:10; Yn 14:23; Yak 4:8; 1 Yoh 2:24; Yud 1:23; Ufu 3:20; Yn 4:24 BWANA yuko karibu na wote wamwitao,
Wote wamwitao kwa uaminifu.
19 1 Yoh 5:14 Hutimiza matakwa ya wote wamchao,
Na pia husikia kilio chao, na huwaokoa.
20 1 Pet 1:5 BWANA huwahifadhi wote wampendao,
Na wote wasio haki atawaangamiza.
21Kinywa changu kitazinena sifa za BWANA;
Wote wenye mwili na walihimidi jina lake takatifu
milele na milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.