Zaburi 43 - Swahili Revised Union Version DC

Sala kwa Mungu wakati wa shida

1 Zab 7:8 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki,

Uniokoe kutoka kwa mtu wa hila asiye haki.

2 Zab 28:7; Isa 26:4 Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?

Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?

3 Zab 2:6; 3:4 Nitumie nuru yako na kweli yako ziniongoze,

Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata katika maskani yako.

4Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye

furaha yangu na shangwe yangu;

Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.

5 Zab 42:5,11 Nafsi yangu, kwa nini kuinama,

Na kufadhaika ndani yangu?

Umtumaini Mungu;

Maana nitamsifu tena,

Aliye msaada wangu,

Na Mungu wangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help