Warumi 12 - Swahili Revised Union Version

Maisha mapya katika Kristo

1 Rum 6:11,13; 1 Pet 2:5; Yn 4:24 Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.

2Efe 4:23; 5:10,17; Rum 1:28; Gal 1:4 Wala msifuate kanuni za dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

3 1 Kor 12:11; Efe 4:7 Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinuie makuu kupita ilivyompasa kunuia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.

41 Kor 12:12 Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;

51 Kor 12:27; Efe 4:25 Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake.

61 Kor 12:4-11 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema tuliyopewa; ikiwa ni unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;

71 Pet 4:10,11 ikiwa ni huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;

8Mt 6:3; 2 Kor 8:2; 9:7 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; msimamizi, na asimamie kwa bidii; anayerehemu, na arehemu kwa furaha.

Sifa za Mkristo

9 1 Pet 1:22; 1 Tim 1:5; Amo 5:15 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkilishika lililo jema.

102 Pet 1:7; Flp 2:3 Kwa pendo la udugu, mpendane ninyi kwa ninyi; kwa heshima mkiwatanguliza wenzenu;

11Ufu 3:15; Mdo 18:25 kwa bidii, bila kulegea; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;

121 The 5:17 kwa tumaini, mkifurahi; katika dhiki, mkisubiri; mkidumu katika kusali;

13Ebr 13:2 kwa mahitaji ya watakatifu, mkifuata ukarimu; katika kukaribisha wageni mkijitahidi.

14Mt 5:44; Lk 6:28; Mdo 7:59; 1 Kor 4:12 Wabarikini wanaowaudhi; barikini, wala msilaani.

15Zab 35:13 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.

16Mit 3:7; Rum 15:5; 11:20 Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinuie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.

17Isa 5:21; 1 The 5:15 Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.

18Mk 9:50; Ebr 12:14 Ikiwezekana, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.

19Kum 32:35; Law 19:18; Mt 5:39; 2 The 1:6,7; Rum 13:4; Ebr 10:30 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.

20Mit 25:21-22; Mt 5:44 Lakini, Adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake.

21Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help