1Ee Mungu, uniokoe,
Ee BWANA, unisaidie hima.
2 Zab 109:29 Waaibike, wafedheheke,
Wanaoitafuta nafsi yangu.
Warudishwe nyuma, watahayarishwe,
Wapendezwao na shari yangu.
3Warudi nyuma, na iwe aibu yao,
Wanaosema, Ewe! Ewe!
4 Isa 61:10; Hab 3:17; Rum 5:2; Flp 3:1; 1 Pet 1:2-9 Washangilie, wakufurahie,
Wote wakutafutao.
Waupendao wokovu wako
Waseme daima, Atukuzwe Mungu.
5 Zab 40:17; Amu 5:28; Zab 141:1; Ebr 10:37; Ufu 22:20 Nami ni maskini na mhitaji,
Ee Mungu, unijilie kwa haraka.
Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu,
Ee BWANA, usikawie.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.