Zaburi 29 - Swahili Revised Union Version

Sauti ya Mungu katika dhorubaZaburi ya Daudi.

1 Zab 96:7-9; 1 Nya 16:28,29 Mpeni BWANA, enyi wana wa Mungu,

Mpeni BWANA utukufu na nguvu;

2Mpeni BWANA utukufu wa jina lake;

Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu.

3Sauti ya BWANA inasikika juu ya maji;

Mungu wa utukufu apiga radi;

BWANA yu juu ya maji mengi.

4Sauti ya BWANA ina nguvu;

Sauti ya BWANA ina utukufu;

5Sauti ya BWANA yaivunja mierezi;

Naam, BWANA aivunjavunja mierezi ya Lebanoni;

6 Zab 114:4; Kum 3:9 Airusharusha Lebanoni kama ndama wa ng'ombe;

Lebanoni na Sirioni kama mwananyati.

7Sauti ya BWANA inatoa miale paa ya moto;

8 Hes 13:26 Sauti ya BWANA yalitetemesha jangwa;

BWANA alitetemesha jangwa la Kadeshi.

9Sauti ya BWANA yawazalisha ayala,

Na kuiacha misitu wazi;

Na ndani ya hekalu lake

Wanasema, Utukufu!

10 Zab 93:4 BWANA aketi juu ya Gharika;

Naam, BWANA ameshika hatamu ya ufalme milele.

11 Isa 40:29 BWANA na awape watu wake nguvu;

BWANA na awabariki watu wake kwa amani.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help