Zaburi 150 - Swahili Revised Union Version

Sifa kwa ukuu Mwingi wa Mungu

1Haleluya.

Msifuni Mungu katika patakatifu pake;

Msifuni katika anga la uweza wake.

2Msifuni kwa matendo yake makuu;

Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3Msifuni kwa mvumo wa baragumu;

Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Kut 15:20; Isa 38:20 Msifuni kwa matari na kucheza;

Msifuni kwa zeze na filimbi;

5Msifuni kwa matoazi yaliayo;

Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Ufu 5:13 Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.

Haleluya.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help